KUTOKA CENTRAL POLISI KAMANDA SIRRO ANAZUNGUMZA
#DawaZaKulevya
'Jumla ya watuhumiwa 16 wamepelekwa mahakamani na majalada yao 24 yapo kwa wakili wa serikali kwa ajili ya uchunguzi.' Sirro
-Watuhumiwa 16 akiwemo Agnes Masongange kesho watapelekwa kwa mkemia mkuu kwa uchunguzi,na ikabainika wanatumia sheria itachukuliwa dhidi yao
-'Tumekamata jumla ya kete 612 za madawa ya kulevya aina ya heroine,puli za bangi 816,misokoto ya bangi 89 na bunda 19 za mirungi..'
-Operesheni ya ukamataji wanaojihusisha na Dawa za Kulevya inaendelea. Jumla ya watuhumiwa 349 wamekamatwa, operesheni ilioyoanza trh 1 Feb. - Kamanda Sirro
-'Watuhumiwa 9 ambao ni Askari polisi wamekabidhiwa kwa Kamishna wa Kupambana na Madawa ya kulevya kwa uchunguzi.'
Akizungumza leo Jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro amesema kati ya watuhumiwa hao, wamo wauzaji, wasafirishaji na watumiaji wa dawa za kulevya, na kwamba wataanza kufikishwa mahakamani siku ya kesho, huku mmoja akipandishwa kizimbani leo.
Pia ametoa taarifa ya kijana mmoja anayedaiwa kusambaza taarifa za uongo, ambapo amesema kuwa jeshi hilo linamshikilia kijana huyo ambaye ni mwanafunzi mwenye umri wa miaka 23, anayedaiwa kutaja majina ya viongozi na kuwatuhumu kuwa wanahusika na dawa na dawa za kulevya.
Kuhusu askari 9 waliotuhumiwa kuhusika na dawa hizo, Kamanda Sirro amesema askari hao wamekabidhiwa kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa ajili ya kuchukuliwa hatua za kisheria.
Kamanda Sirro amesema hadi sasa jumla ya kete 612 pamoja na bangi vimekamatwa na kwamba kuna watu wengine 17 ambao bado jeshi hilo linawafuatilia na watakuwa mbaroni wakati wowote.
'Jumla ya watuhumiwa 16 wamepelekwa mahakamani na majalada yao 24 yapo kwa wakili wa serikali kwa ajili ya uchunguzi.' Sirro
-Watuhumiwa 16 akiwemo Agnes Masongange kesho watapelekwa kwa mkemia mkuu kwa uchunguzi,na ikabainika wanatumia sheria itachukuliwa dhidi yao
-'Tumekamata jumla ya kete 612 za madawa ya kulevya aina ya heroine,puli za bangi 816,misokoto ya bangi 89 na bunda 19 za mirungi..'
-Operesheni ya ukamataji wanaojihusisha na Dawa za Kulevya inaendelea. Jumla ya watuhumiwa 349 wamekamatwa, operesheni ilioyoanza trh 1 Feb. - Kamanda Sirro
-'Watuhumiwa 9 ambao ni Askari polisi wamekabidhiwa kwa Kamishna wa Kupambana na Madawa ya kulevya kwa uchunguzi.'
Akizungumza leo Jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro amesema kati ya watuhumiwa hao, wamo wauzaji, wasafirishaji na watumiaji wa dawa za kulevya, na kwamba wataanza kufikishwa mahakamani siku ya kesho, huku mmoja akipandishwa kizimbani leo.
Pia ametoa taarifa ya kijana mmoja anayedaiwa kusambaza taarifa za uongo, ambapo amesema kuwa jeshi hilo linamshikilia kijana huyo ambaye ni mwanafunzi mwenye umri wa miaka 23, anayedaiwa kutaja majina ya viongozi na kuwatuhumu kuwa wanahusika na dawa na dawa za kulevya.
Kuhusu askari 9 waliotuhumiwa kuhusika na dawa hizo, Kamanda Sirro amesema askari hao wamekabidhiwa kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa ajili ya kuchukuliwa hatua za kisheria.
Kamanda Sirro amesema hadi sasa jumla ya kete 612 pamoja na bangi vimekamatwa na kwamba kuna watu wengine 17 ambao bado jeshi hilo linawafuatilia na watakuwa mbaroni wakati wowote.
No comments:
Post a Comment