Friday, December 16, 2016

Watoto elfu 17 waandikishwa kama askari watoto kwenye mgogoro nchini Sudan Kusini

Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF limesema, tangu mgogoro wa kijeshi ulipotokea nchini Sudan Kusini miaka mitatu iliyopita, watoto elfu 17 wameandikishwa kwenye makundi ya wapinzani askari watoto.

Takwimu zilizotolewa na shirika hilo zimeonyesha kuwa, mpaka sasa ni askari watoto 1,932 tu wameachiwa huru.

Kuanzia mwaka huu, Shirika hilo na mashirika mengine yamepokea watoto laki 1.8 wanaokabiliwa na utapiamlo, na idadi hii imeongezeka kwa asilimia 50 kuliko mwaka jana.
 

Tuesday, December 13, 2016

Japan yatuma mtambo wa kufagia anga za juu

 

Japan imezindua chombo cha anga za juu ambacho kitabeba mtambo maalum wa kukusanya taka kutoka anga za juu.

Chombo hicho kitakuwa na nyaya ndefu za urefu wa mita 700 (nusu maili) ambazo zitatumiwa kuokota taka hizo. Nyaya hizo zitaundwa kwa madini ya aluminiamu na chuma cha pua.

Mtambo huo umeundwa kwa usaidizi kutoka kwa kampuni ya uvuvi.
Inakadiriwa kwamba kuna zaidi ya vipande 100 milioni vya taka kwenye mzingo wa dunia.
Mpango wa kupeleka watu wakaishi Mars
Kifaa kutoka angani chaanguka Myanmar

Vipande hivi ni pamoja na vipande vya setilaini zilizoacha kutumika, vifaa na vipande vya roketi.

Vipand vingi kati ya hivi vinasonga kwa kasi sana kuizunguka dunia kwenye mzingo wake, baadhi vikifikia kasi ya kilomita 28,000 kwa saa (maili 17,500 kwa saa) na kuna wasiwasi kwamba vinaweza kusababisha ajali mbaya au kuharibu mitambo inayosaidia mawasiliano duniani.
 
Taka hizo zimerundikana katika kipindi cha miaka 50 tangu binadamu aweze kuruka kwenya anga za juu, setilaiti ya Sputnik iliporushwa anga za juu na Muungano wa Usovieti mwaka 1957.

Mgongano kati ya setilaiti na kufanyiwa majaribio kwa mitambo ya kujikinga dhidi ya mshambulio ya setilaiti vimezidisha tatizo la taka anga za juu.


Chombo hicho cha Japani kimepewa jina Kounotori na kinaundiwa katika kituo cha anga za juu cha Tanegashima
 
Roketi ya H-IIB iliyobeba  chombo cha Kounotori ikipaa angani baada ya kurushwa kutoka kituo cha anga za juu cha Tanegashima tarehe 9 desemba



Chombo hicho kilichopewa jina Kounotori (Korongo kwa Kijapani) na ambacho kimebebea mtambo huo, kilipaa kutoka kituo cha safari za anga za juu cha Tanegashima, kaskazini mwa bahari ya Pasifiki Ijumaa kuelekea kituo cha kimataifa cha anga za juu.

Watafiti wanasema nyaya hizo zinazotumia nguvu za maalum za sumaku ambazo kwa Kiingereza huitwa electro-dynamic, kitazalisha nguzu za kutosha kubadili mwelekeo wa vipande hivyo na kuvielekeza kwenye anga ya dunia ambapo vitateketea.
Mataifa ya Ulaya kutuma chombo sayari ya Mars
Roketi kubwa ya Uchina yafanya safari ya kwanza

Kampuni ya wataalamu wa kuunda nyavu za kutumiwa na wavuvi Nitto Seimo Co, ambayo imekuwepo kwa miaka 106, imeshirikiana na shirika la anga za juu la Japan kuunda mtambo huo.

Majaribio ya kutumia mtambo huo ni moja ya juhudi za kuhakikisha anga za juu ni salama kwa wana anga kwa kupunguza taka.
Inatarajiwa kwamba itasaidia kulinga vituo vilivyo anga za juu pamoja na setilaiti za kutabiri hali ya hewa na zile zinazotumiwa kwa mawasiliano, vyote vya thamani ya mabilioni ya dola. Image copyright Getty Images

Waziri Nchemba: Maiti Saba wa Mto Ruvu ni wahamiaji haramu

 Mheshimiwa Mwigulu NCHEMBA (wewe ni waziri wa mambo ya ndani ya nchi)..,
.., leo asubuhi ulikuwa katika kipindi cha Tuongee Asubuhi kinachorushwa na kituo cha matangazo cha Star TV.., nimekusikia kauli zako, kuhusu 'issue' ya watu wale 7 waliokutwa mto Ruvu wakiwa wamekufa (vifo vya ajabu), umesema kwamba watu wale ni WAHAMIAJI HARAMU .., mimi nikuulize maswali yafuatayo;
(i) Je, wahamiaji haramu ndiyo wanapaswa kuuwawa na kutupwa mto Ruvu!?
(ii) wahamiaji haramu ndiyo wanapaswa kujeruhiwa kwa vitu vyenye ncha kali na kuuawa!?
(iii) wahamiaji haramu ndiyo wanatakiwa kuuwawa na kufungwa kwenye mifuko ya Sandarusi na kuwekwa mawe ndani!?
(iv) sheria za nchi, sheria za jeshi la polisi, sheria za idara ya uhamiaji zinasema nini kuhusu wahamiaji haramu.., kuuwawa!?
(v) kama kweli ni wahamiaji haramu.., nani ametoa idhini ya kuwaua, nani amewaua, na kwanini watupwe mto Ruvu wakiwa wamefungwa kwenye mifuko na mawe ndani yake!?
.., niendelee kukuliza mheshimiwa waziri.., hao wahamiaji haramu, wanatoka katika nchi gani.., Je, nchi zao zikigundua kwamba mliwaua watu wao na kuwazika huko Bagamoyo, hauoni mnaleta mgogoro mkubwa wa kidiplomasia!?
Mheshimiwa waziri, kazi ya jeshi la polisi ni kulinda watu na mali zao, kuhakikisha usalama wa raia ni kiwango cha juu, bila kuhatarisha usalama wao, maana wao ndiyo kipaumbele cha kwanza cha serikali (walipa kodi)..,
.., umetoa ufafanuzi hafifu sana kuhusu suala la kupotea kwa Ben Saanane na kutoonekana kwa kitambo kirefu.., kuna maswali ya kuoanisha hapa;
(i) kwanini ile miili 7 iliyokutwa kule Ruvu izikwe kwa haraka ile na halmashauri!?
(ii) kwanini jeshi la polisi, halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo hawakutaka kufanya uchunguzi kubaini nini chanzo!?
(iii) kwanini jeshi la polisi liko kimya hadi sasa, wiki nzima, hadi 'pressure' ya watanzania inakuibua wewe waziri, tena kwa kuulizwa!?
(iv) Je, wakati huu ndugu, jamaa, rafiki wa Ben Saanane wakiwa katika sintofahamu ya ndugu yao, kwanini Jeshi la polisi halikuona umuhimu wa kutokuzika maiti zile kwa haraka ile!?
(v) kuna kila sababu ya kumtaka OCD wa Bagamoyo na vyombo vya ulinzi na usalama katika halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo, kutoa kauli yenye kueleweka.., (wako chini ya ofisi yako hawa watu)
NB; Pia.., kuna habari moja iliwahi kutangazwa na ITV mwezi wa August, mwaka 2016, naomba kunukuu sehemu ya habari ile..,
".., Zaidi ya watanzania 56 katika vijiji vya Chamchuzi na Buguluka vilivyoko katika kata ya Bwelanyange iliyoko wilayani Karagwe mkoani Kagera waliokuwa wakijihusisha na shughuli za uvuvi ndani ya mto Kagera na ziwa hiema wanadaiwa kutekwa na kuuawa kikatili na watu wanaodhaniwa kuwa ni askari wa nchi jirani Rwanda ambao mara kwa mara hufanya doria ndani ya mto huo na ziwa hilo. "
.., kitu cha kusikitisha sana.., serikali kupitia wizara ya mambo ya ndani ya nchi.., haikuwahi kutoa kauli, taarifa yoyote juu ya habari hiyo.., mbaya sana!
Mwisho ;
Jeshi la polisi kupitia intelejensia yake, wanapaswa kuwa 'proactive' kuliko kuwa 'reactive' kwenye masuala ya ulinzi wa mali za umma na usalama wa raia.., intelejensia ya jeshi la polisi inatakiwa kufanya kazi kubwa kabla umma kupiga kelele ndiyo wao wachukue hatua.., (kama jeshi la polisi linaweza kubaini kuhusu vurugu kutokea katika mkutano wa kisiasa ambao haujafanyika.., linashindwa nini kubaini usalama wa raia na mali zao!?)
matukio ya watanzania kuuwawa yamekuwa yakiongezeka kila kunapokucha, watanzania 9 katika wilaya ya Kyelwa waliokuwa wakifanya shughuli za uvuvi ndani ya mto Kagera waliuwawa na watu wanaodhaniwa askari wa nchi jirani ya Rwanda hali ambayo ilikusikitisha wewe (waziriwa mambo ya ndani) wakati huo ukiwa katika ziara ya kikazi katika mkoa wa Kagera.., (lakini wizara yako haikutaka kutoka mbele ya watanzania na kusema kitu, kuhusu matukio hayo)
Jeshi la polisi linapawa kuwa jeshi la kulinda raia na mali zao.., siyo jeshi la kulinda maslahi ya watu wachache sana katika Jamhuri ya muungano wa Tanzania.., tazama, raia wanakufa vifo vya ajabu katika nchi yao, zinatoka kauli rahisi, kwamba ni wahamiaji haramu.., siyo sahihi.., tunapaswa kupata ukweli dhidi ya maiti zile zilzokutwa katika mto Ruvu.., pia tuelezwe;
(i) kwanini zitupwe mto Ruvu.
(ii) kwanini zifungwe na mawe ndani.
(iii) kwanini zifungwe katika mifuko ya Sandarusi.
(iv) kwanini zionekane kujeruhiwa na vitu vyenye ncha kali.
(v) kwanini mamlaka za usalama ziko kimya..,
Ahsante,
Mwananchi wa kawaida,
Martin Maranja Masese (MMM)
Source JF
waziri wa mabo ya ndani Ndg Mwigulu Nchemba

Monday, December 12, 2016

CHAMBUA MATAMKO YAFUATAYO...

#PART ONE:
1. WAZIRI WA VIWANDA, MWIJAGE "...tulikuwa tunaficha tu, ukweli ni kuwa DANGOTE anataka apewe GESI bure, nchi hii siyo shamba la Bibi"
2. WAZIRI WA NISHATI, MUHONGO "...DANGOTE hawasemi ukweli, gharama na Makaa ya Mawe ya Tanzania ni nafuu kuliko ya Afrika Kusini, hebu naomba wawaeleze ukweli"

3. TPDC: "...Shirika la Maendeleo la Petroli Tanzania (TPDC) linapenda kukanusha taarifa zinazoenezwa na Kampuni ya Dangote pamoja na washirika wake kupitia mitandao ya kijamii.....Kiwanda cha Dangote kimeomba kupewa gesi asilia kwa bei ambayo hapa kwetu Tanzania ni kidogo kwani kiasi hicho cha bei ndicho kinacholipwa kununulia gesi ghafi kutoka kisimani.... Taarifa hizo (Za Dangote) hazina mantiki yoyote na zinapaswa kupuuzwa...."

4. RAIS JPM: "...Kuna ujanja ujanja unatumika kumuuzia GESI Dangote kwa faida ya wachache, kuanzia sasa wasiliana na serikali moja kwa moja...."

5. DANGOTE: "...Hapakuwa na tatizo lolote, kila kitu kinakwenda sawasawa...".
#PART TWO:
1. WAZIRI MWIGULU NCHEMBA: "...miili iliyookotwa ni ya wahamiaji haramu..."

2. WAZIRI MKUU, KASIMU MAJALIWA: "Miili iliyookotwa inahusishwa na masuala ya Ugaidi..."
3. WAZIRI MKUU, KASIMU MAJALIWA: "Naagiza Uchunguzi mara moja (akiielekeza Wizara ya Mwigulu".

SOMO LA MAISHA KUTOKA KWENYE WARAKA WA SERENA

VITA ya ubaguzi wa kijinsia kwenye malipo ya wacheza tenisi imepamba vyombo vingi vya habari mwanzoni mwa mwaka huu, huku mmoja wa nyota wa kike wa mchezo huo waliopigia kelele sana suala hilo, Serena Williams, akizidi kulivalia njuga.

Moja ya mfano aliotoa Serena kuonyesha kuna ubaguzi wa kijinsia kwenye mchezo huo ni pale wanapomtaja kama mwanamichezo bora wa kike, badala ya kusema mmoja wa wanamichezo bora.

Mshindi huyo wa mataji makubwa 22, ameweka wazi kuhusiana na hilo kwenye barua yake ya wazi iliyochapishwa na jarida la Porter.

Mwanzoni mwa mwaka huu, mchezaji wa zamani wa tenisi, Ray Moore, ambaye pia ni mwandaaji wa michuano mbalimbali ya mchezo huo kama Paribas Open, California, alisema kwamba wachezaji wa kike wa mchezo huo wanapaswa kuwashukuru Roger Federer na Rafael Nadal kuubeba mchezo huo.

Lakini Serena alimpinga wazi mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 70, kabla ya baadaye kuandika waraka mkubwa.

Serena aliandika katika waraka wake: “Nimekuwa na bahati kuwa kwenye familia ambayo inaunga mkono ndoto zangu na kunitia moyo.”

“Nimejifunza kutokuogopa. Nimejifunza umuhimu wa kupigania ndoto zangu, jambo la msingi likiwa ni kufikiria makubwa zaidi. Vita yangu ilianza nikiwa na umri wa miaka mitatu na tangu hapo sijakata tamaa.

“Lakini kama tunavyojua, mara nyingi wanawake hawapewi kipaumbele cha kutosha au kukatishwa tamaa kwa kile wanachokichagua. Naamini pamoja tunaweza kubadilisha hilo. Kwangu mimi ilikuwa ni suala la ujasiri.

“Kile wengine walichoona kama ni kosa au kutokuwa na faida, lakini kwa upande wangu, vita yangu, jinsi yangu vilichochewa na mafanikio yangu. Kamwe sikuruhusu kitu chochote au mtu kunifanya nishindwe.

“Wakati suala la kulipwa sawa na wanaume linapokuja, linanikera sana kwa kuwa najua kila kitu kama mtu mwingine, tumefanya kazi moja na kujitoa sawasawa kama wanavyofanya wanaume. Sitapenda binti yangu alipwe kidogo kuliko mtoto wangu wa kiume kwa kazi moja wanayoifanya. Au wewe utapenda. Siwezi kunyamaza.”

Pia Serena alishangaa suala la kuingiza jinsi yake kwenye kutaja mchezo wake kati ya wachezaji wengine, huku Federer akiwekwa pamoja na mchezaji wa gofu Tiger Woods na nyota wa mpira wa kikapu, LeBron James.

“Kama mnavyojua wanawake wanapitia vikwazo vingi mpaka kuweza kufikia mafanikio,” aliandika Serena.

“Vikwazo vinaendelea kuwapo siku zote kwa wanawake. Watu huniita wa wanamichezo wakubwa wa ‘kike’ duniani.’ Je, wanasema LeBron ni mmoja wa wanamichezo bora wa kiume? Vipi kwaTiger? Federer? Kwanini wao wasiitwe hivyo? Kwa kuwa wao si wa kike. Tuhukumiwe na mafanikio yetu sio na jinsi zetu.

“Katika kila kitu nilichofanikiwa kwenye maisha yangu, nashukuru nimepitia milima na mabonde ambayo inakuja na mafanikio. Ni matumaini kwamba historia yangu na ya kwako itawatia moyo wanawake wengi kupambana kwa ajili ya mafanikio na kutimiza ndoto zao. Lazima tuwe na maono makubwa ili kukitia moyo kizazi kijacho cha wanawake ili kuweza kupambana.”
 

Wednesday, December 7, 2016

Waziri wa afya wa Tanzania atahadharisha juu ya mlipuko mpya wa kipindupindu

Waziri wa afya wa Tanzania Bw Ummy Mwalimu ametahadharisha kuhusu mlipuko mpya wa ugonjwa wa kipindupindu nchini humo.

Bibi Mwalimu amewataka maofisa wa afya kutekeleza taratibu zinazolenga kusimamia maambukizi ya ugonjwa huo na kuanzisha kampeni ya kuelimisha umma kuhusu ugonjwa huo.

Ripoti mpya iliyotolewa na wizara hiyo inaonesha kuwa watu 6 wamefariki dunia na wengine 458 wameripotiwa kuambukizwa ugonjwa huo mwezi Novemba, na maeneo yaliyoathiriwa zaidi na Morogoro, Dodoma, Mara, Kigoma, Arusha na Dar es Salaam.
Bibi Mwalimu amesema ugonjwa huo hutokana na uchafu, na baadhi ya watu wana desturi ya kuchafua vyanzo vya maji.

waziri ummi akizungumza na waandishi wa habari

MATAPELI WAKUBWA WANNE (4)KUWAHI KUTOKEA TANZANIA : 

 
1..DAUDI BALALI... Nahisi huyu ni mmoja kati ya watanzania magenious zaidi kuwahi kutokea. Huyu kipindi anasoma alirushwa sana madarasa kutokana n kiwango kikubwa cha akili. Hii ilipelekea yeye kusoma elimu ya msingi na secondary kwa miaka 10 tu. Akiwa na miaka 18 alijiunga na chuo kikuu cha Howard marekani ambapo alitunukiwa shahada yake ya kwanza. Akiwa na miaka 25 alitunukiwa PHD.. Kisha akarudi nchini kuwa mchumi wa bank kuu mwaka 1967.. Baadae kidogo akaajiliwa IMF ambako alifanya kazi kwa miaka 23 kabla ya mkapa kumrudisha nchini kama mshauri wake wa masuala ya uchumi na baadae kumfanya gavana wa bank kuu.
Kilichofanya kuwepo kwenye list hii ni tukio alilofanya la ukwapuaji wa BILLION 164 za kitanzania pale bank kuu..
Nafahamu kuna theories nyingi sana kuhusu ufisadi wa EPA lakini kwa mujibu wa serikali ni kuwa BALALI alikula njama yeye na wale wafanyabiashara wakakwapua fedha pasipo serikali kujua, kwa maana hiyo BALALI alimpiga changa la macho Waziri mighiro, Rais, na hata usalama wa taifa..... ALIWEZA
2..MANYAUNYAU
Huyu jamaa tunafahamu alitikisa sana miaka ya 2006 hadi 2008 alijigamba kuwa akinywa damu ya Paka anapta uwezo wa kimiujiza kufichua wachawi. Alizunguka mitaa karibia yote ya uswahilini dar (uzunguni alipatenga) baada ya kuteka Hisia za watu vya kutosha akaanza na ziara za mikoani.
Jamaa akaingiza mkwanja mrefu sana kwa kazi yake hii nakumbuka miaka ile ya 2008 alishanunua RAV4 Kali na mjengo wa maana.... Sijui kwa sasa amepotelea wapi!
3..ALEX MASSAWE
Huyu jamaa ni tapeli(first class) alikuwa anatapeli kuanzia raia wenzake, serikali, mashirika mpaka matajiri wakubwa. Alitapeli sana watu nyumba, magari, mashamba na hata fedha, serikali iliangaika sana na huyu jamaa kwa miaka kadhaa lakini hawakufua dafu, mpaka interpol walipomkamata huko dubai.
Inasemekana jamaa alikuwa a napiga dili zake na watu wazito serikaln na bungeni. Inasemekana kuna wabunge watatu kutoka mkoa mmoja wa kaskazini ndio alikuwa anapiga nao sana ishu za madili ya gari za wizi na kusafisha fedha haramu..
4..BABU WA LOLIONDO
Mpaka Leo hii bado sijaelewa babu aliwezaje kuwapiga changa kiasi Kile, hivi ni kwamba babu alikuwa kichwa sana au media ilisaidia. Kipindi kile kuna watu walitamani BABU atangazwe kama nabii au shujaa wa taifa, mpaka wa kuu wa nchi walitengeneza hadi kiwanja kidogo cha ndege wakawa wanatua, wanapanga foleni, wanapiga magoti kwa unyenyekevu na kuachama midomo kama wanakula sakramenti takatifu.. Kila Kona ilikuwa BABU, BABU, BABUUUUU...
kila mtu kuanzia raia hadi viongozi wakubwa walikuwa wanapigania KIKOMBE kwa mchango (sadaka) ya mia tano tano (500)na ghafla ikawa ziiiiii Babu kimyaaaa




matukio ktk picha
 
GODBLESS LEMA......
https://www.facebook.com/100008744220984/videos/1628725077428951/

Thursday, December 1, 2016


UFAFANUZI WA KAULI YA PAUL MAKONDA.

Na:Goodluck Abel 
"Msinijaribu, ardhi kinondoni nitawashughulikia, hadi mtajuta kuzaliwa. 'Mimi nikisimama hapa, amesimama Mungu', sikuletwa hapa kwa bahati mbaya, nitawatia ndani wote, na hakuna mtetezi wenu, wewe mama unanisikia? hauna wa kukutetea.."

Kauli hiyo imetolewa na kijana wa UVCCM aliyeteuliwa na Rais Magufuli kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam ili kuwakomesha wapinzani, Ndg. Paul Makonda.

Ili kuelewa, ni vema kutafakari neno kwa neno, kama ifuatavyo;

1. "Mtajuta kuzaliwa", kujuta kuzaliwa ni hatua ya mwisho ambayo binadamu huifikia hata akamuuliza muumba wake ni kwanini alimuumba, hivyo Makonda anajivika cheo cha muumbaji.

2. " Hakuna wa kuwatetea", kwamba akiamuru yeye, maamuzi yake ni ya mwisho. Lakini katiba na sheria za nchi zinamruhusu mtu kujieleza (natural Justice), na kuwa na utetezi dhidi ya mashitaka yake mahakamani, hivyo: kwa amri ya Makonda, akikuweka ndani unaweza kuozea huko na hakuna wa kukutetea.

3. "Nitawashughulikia", maana yake atatoa adhabu, ambapo katiba ya nchi inasema kuwa mtu hatoadhibiwa kwa kosa lolote, hata la jinai, mpaka itakapothibitika mahakamani kuwa ana kosa, hivyo: Makonda ndiyo mwenye mamlaka na maamuzi ya mwisho juu ya hukumu ya mtu na sio mahakama tena.

4. " Mimi nikisimama hapa, amesimama Mungu", #Astaghfirullah... Yaani Makonda sasa anachukua nafasi ya Mungu, kwa hili nashindwa kufafanua zaidi, naishia kutamka tena 'Astaghfirullah' yaani 'Mungu asamehe'.

5. "Sikuletwa hapa kwa bahati mbaya", hili: kwa bahati mbaya hatufahmu kuna nini nyuma ya pazia hata yeye mwenyewe kukiri kuwa hakuletwa kwa bahati mbaya, maana yake lipo kusudi, na matokeo ya kusudi hilo ni hayo yaonekanayo, mbali na aliyemteua kusema kuwa "nimekuongeza cheo ili kuwakomesha wapinzani wako"

Hapa ndipo tulipofikia mtanzania mwenzangu, tufahamu kuwa nchi yetu ikiupoteza utawala bora unaozingatia sheria za nchi na katiba yetu wenyewe, nchi itatumbukia pabaya siku za usoni.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI;

Imetolewa na Afisa mawasiliano na Uchaguzi –CUF TAIFA, 29 Novemba 2016.

"DHAMBI YA USALITI INAMTESA LIPUMBA".

Jana tarehe 28/11/2016 Lipumba alizungumza na waandishi wa habari kwa kile alichokiita kujibu hoja za Katibu Mkuu wa Chama Maalim Seif Sharif Hamad alizotoa katika mkutano na wahariri na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari vya ndani na nje ya nchi.
Tunasikitika kusema kuwa Lipumba ameshindwa kujibu hoja na badala yake amejikita kwenye majigambo na kujifaharisha na waganga wa kienyeji na vyombo vya dola kuwa wamemuhakikishia ataendelea kuwa Mwenyekiti wa CUF mpaka mwaka 2019.

Kwanza tunawashukuru watanzania kwa kuendelea kumpuuza kwani yapo masuala mengi yanayowasumbua watanzania kama kuyumba kwa uchumi na serikali ya awamu ya tano ambayo Lipumba alijenga ubia nayo tangu kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka jana ikiwa ni pamoja na mwendelezo wa urafiki wa kuihujumu CUF.

Ndiyo maana hivi sasa anashindwa kufungua mdomo wake kukosoa na kushauri hadhara njia mbadala za kuondokana na hali hii badala yake anampongeza Mheshimiwa Rais Magufuli na serikali yake kwa kuharibu uchumi wa nchi. Lipumba huyu siyo yule tuliyekuwa tunamfahamu. Na haya ndiyo madhara na gharama ya kuwa kibaraka wa mfumo kandamizi wa demokrasia.

Ameshindwa kujibu hoja na ameshindwa kukanusha juu ya uhusiano wake na Jeshi la polisi nchini ambao umekuwa ngazi ya kuhujumu Chama huku vitendo vya kihalifu vya Lipumba na wapambe ake vikikingiwa kifua. Amejitwika jukumu la kuwa msemaji wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini na kushindwa kupinga hoja ya jaribio la kutaka kuiba fedha za ruzuku za Chama kwa kutaka kufungua akaunti binafsi akishirikiana na Jaji Francis Mutungi. Ameshindwa kujibu hoja kuwa wapambe na wahuni wake wanafanya uhalifu na kulindwa na Polisi na bila kuchukuliwa hatua zozote. Lakini pia hajawaambia Watanzania sababu za kujiuzulu kwake na sababu za kutaka kulazimisha tena kuendelea kuwa Mwenyekiti wa The Civic United Front (CUF-Chama Cha Wananchi).

Lipumba anajidhalilisha na kujivunjia heshima na mwenye njaa ya ruzuku ni yeye aliyetaka kufungua akaunti yenye jina la chama ili ajichukulie fedha za chama kinyume na taratibu na hali akijua hana mamlaka ya kufanya hivyo.

Hata kama angekuwa ni ‘Mwenyekiti Halali wa Chama’ kwa mujibu wa Katiba ya CUF; Majukumu ya Mwenyekiti wa Chama Taifa yamebainishwa katika ukurasa wa 82 Ibara ya 91(1)(a-m) ambayo hayampi mamlaka ya kufanya haya anayoyafanya Lipumba ikiwemo kutaka kudhibiti fedha na mali za Chama.

Katiba ya CUF ambayo yeye anadai na kusisitiza kutaka ifuatwe kwa kuiangalia zaidi Ibara ya 117(2) pekee, imempa Majukumu muhimu Katibu Mkuu wa Chama katika ukurasa wa 85 Ibara ya 93(1)(a-k)(2) kuwa;
a) “Atakuwa Mtendaji Mkuu wa Chama na pia mwajibikaji mkuu wa shughuli zote za utendaji za Chama kitaifa” Ibara ya 93(1)(a).

b) "Atakuwa na dhamana ya ofisi za Makao Makuu na Ofisi Kuu ya Chama” Ibara ya 93(1),(f)

c) "Atakuwa mwajibikaji mkuu wa mambo yote ya fedha na mali za Chama katika ngazi ya Taifa (Chief Accounting Officer)” Ibara ya 93(1),(i).

Kwa hiyo, kitendo cha Katibu Maalim Seif, kuhoji juu ya UHUNI wa Jaji Mutungi wa kuzuia RUZUKU ya CUF kwa sababu Mutungi aliona haitamfikia Lipumba ili kutumika kwa malengo ya dola kuisambaratisha CUF, ni kitendo muhimu sana kikatiba, ni kitendo kinachodhihirisha kuwa Katibu Mkuu anatimiza wajibu wake kama Msimamizi Mkuu wa masuala ya fedha za chama. Kama ni njaa anayo BWANA YULE, ambaye alipokwenda Lindi na Mtwara alibeba vimemo na kuingia benki ya NMB tawi hatulitaji na kupewa Tzs 20,000,000 kwa maelekezo ya kada na kiongozi maarufu wa CCM. Wafanyakazi wa Tawi hilo la NMB hadi leo hawaamini inakuwaje kiongozi wa Upinzani aliyejitambulisha kama anayepambana na CCM, kupewa mamilioni ya pesa na viongozi wa CCM.

Njaa! Kama kuna mwanasiasa ana njaa na ametumia maisha yake kutumika ni Lipumba. Lipumba na wahuni wake wakumbushwe juu ya hotuba zake mwaka 2011 baada ya Kikwete kushinda ushindi mwembamba. Lipumba hajawajibu watanzania alikuwa na maana gani kusema "aliokoa jahazi ili Kikwete ashinde uchaguzi" ilihali Lipumba alikuwa mgombea wa CUF. Je,ni kikao gani cha CUF kilimtuma Lipumba akaokoe jahazi na kumpa ushindi Kikwete mwaka 2010?

Lipumba amepoteza weledi wake wa mambo tuliokuwa tunaujua hapo kabla, anazungumza mambo bila Takwimu, bila ushahidi. CUF kama taasisi makini, taasisi Imara imeshafanya maamuzi kupitia vikao halali vya Chama Mkutano Mkuu Taifa na Baraza Kuu la Uongozi Taifa, Katibu Mkuu Maalim Seif Sharif Hamad hana mamlaka ya kuzungumza na Lipumba na kulipatia ufumbuzi suala hili kwa kuwa si lake ni la Chama na Chama kilishafanya maamuzi ya kumvua uanachama. Kazi aliyojipa kwa kupewa bahshishi na washirika wake ya kuvuruga upinzani haitafanikiwa kwa sababu CUF na vyama washirika itaendeleza ushirikiano na kuondoa mapungufu yote yaliyojitokeza katika uchaguzi uliopita ili tuwe na nguvu madhubuti ya pamoja kukabiliana na CCM katika chaguzi zijazo. Kamwe hataweza kuturudisha nyuma na kutuyumbisha.

Lipumba anazungumzia ujumbe wa Maalimu Seif kupitia barua pepe yake ya Disemba 30, 2015 eti kuwa anamtambua! Hii inatia shida kidogo kumuelewa Lipumba, alisema ataendelea kuwa mwanachama wa kawaida na kadi yake amelipia mpaka mwa 2020, sasa kutumiwa ujumbe ndio imemaanisha kuwa yeye ni ‘Mwenyekiti Halali’ na inadhihirisha kuwa Maalim Seif hana ugomvi binafsi yeye. Inastaajabisha sana kuona kuwa aliyekuwa kiongozi wa kupinga propaganda za CCM leo anatumia propaganda hizohizo dhidi ya Chama cha CUF kutaka kuwabagua watanzania kwa misingi ya udini, ukanda, utanganyika na uzanzibari.

Wakati Maalim Seif anajenga hoja za matukio takribani tisa yaliyotokea katika kipindi cha baina ya Mwezi Agosti-Novemba, 2016 ikiwemo jaribio la utekaji na Jeshi la Polisi kushindwa kutekeleza wajibu wake, yeye amejitokeza kuwa msemaji pia wa jeshi la Polisi, kwa kweli inasikitisha sana. Lipumba aache kuwa na uchu wa madaraka zama zake zimekwisha ndani ya CUF, kutamani kwake kugombea nafasi ya Urais mwaka jana kuliathiriwa na hali halisi ya mazingira na haja ya wakati ule na hayakuruhusu kabisa kwake kuwa mgombea na kufanya vizuri. Eti Lipumba haoni mchango wa Mhe. Edward Lowassa katika UKAWA! Je? Dhamira na nafsi yake zimeacha kumsuta? Mhe. Edward Lowassa amepata asilimia 39 ya kura, Lipumba anakataa kuwa Lowassa hana mchango kwenye mabadiliko ya demokrasia nchini? Lipumba alizoea kupata asilimia 7 ya kura na alijenga ufalme akidhani kuwa ataendelea kuwapiga mnada watanzania na kuchukua hela ili "kuokoa ahazi" kila chaguzi utakapofika?

Kwa upande wa Zanzibar CUF tumeshinda nafasi ya Urais na kushuhudia CCM na Dola wakipora ushindi huo kwa kumtumia Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar –ZEC. Lipumba anakataa? Anaunga mkono maamuzi ya mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi Zanzibar ZEC? Lipumba anachukia ikielezwa kuwa Mhe. Edward Lowassa amemshinda Magufuli katika matokeo ya kura za Urais Zanzibar!

Kushirikiana na vyama vingine vya siasa ni maamuzi yanayotokana na kikao cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa ambalo bado linatambua uwepo wa ushirikiano wa vyama–UKAWA. Je yeye binafsi kama angekuwa Mwenyekiti wa CUF Taifa anao uwezo wa kuiondoa CUF katika UKAWA bila kutumia njia za vikao? Mashirikiano haya yanaendelea katika uundaji wa Halmashauri na CUF kuwa na Mameya na Manaibu Meya Je kwa akili ya Lipumba Mameya na Manaibu Meya hawa wajiuzuru ili wasishirikiane na CHADEMA? Aleze sababu za kulazimisha kutaka kuwa mwenyekiti ni zipi wakati alijiuzuru kwa matashi yake binafsi mbali na kuombwa asifanye hivyo? Iweje viongozi wa Dini na wa Chama waliomuomba sana wakati ule asijiuzulu akawakatalia katakata na kuendelea na dhamira yake na hatimaye akakimbia vita na kukiacha chama katika kipindi kigumu cha maandalizi ya uchaguzi mkuu, ilhali leo anadai amezingatia maombi ya viongozi wa dini wale aliowakatalia mwanzo? anadai kuwa alimuandikia barua Katibu Mkuu akajibiwa kuwa asubiri, kwani kwa akili ya Lipumba, kurudi kwake kwenye nafasi ya Uenyekiti wa Chama kwa mujibu wa katiba ya CUF yanafanywa na Katibu Mkuu wa Chama? Huu ni umbumbumbu wa sheria na Katiba ya CUF wa hali ya juu.

Kwa mashirikiano ya CUF na vyama vingine tumeweza kufanya kampeni za uhakika na za kisasa zilizoleta ushindani mkubwa na kuifanya CUF ipate wabunge katika majimbo kumi (10) ya Tanzania Bara na kuongoza Halmashauri nne (4) nchini. Lipumba anakataa na kupinga kuwa hatukupata wabunge 10? Je, anakumbuka kuwa miaka yake 19 ya Uenyekiti wa CUF chama hakikuwahi kuwa na wabunge hata watatu? Leo CUF ina halmashari 4 na madiwani zaidi ya 300, miaka 19 ya Uenyekiti wa Lipumba ndani ya CUF iliwahi kuleta hata halmashauri moja?

Lipumba ametakiwa aeleze sababu za kujiuzuru kwake ni zipi? lakini ameshindwa kufanya hivyo. Lipumba anazeeka vibaya na amekuwa msahaulifu, anapozungumza katika vikao vyake vya ndani maeneo mbalimbali anasema Wazanzibar hawamtaki na kwamba wanataka kujitoa katika makucha ya Wazanzibari, anazungumzia Utanganyika na Uzanzibari, na wapambe wake wanalishikilia bango suala hili. Aache kueneza na kupandikiza chuki kwani ajenda hizo ndizo zimefanya miaka yake 19 ya uongozi ndani ya CUF kukosa lolote la kujivunia.

KUHUSU SUALA LA UMOJA WA KATIBA YA WANANCHI-(UKAWA):

Lipumba ameulizwa na kushindwa kujibu, nani aliyeleta UKAWA ndani ya CUF? Nani aliyeweka saini za makubaliano ya UKAWA pale Jangwani? UKAWA umeanzia Bunge la Katiba. Katibu Mkuu Maalim Seif hakuwa mjumbe wa Bunge la Katiba. Yeye Lipumba ndiye aliyekwenda kumuona Mheshimiwa Lowassa na kumtaka ikiwa CCM itamuengua ajiunge na UKAWA. Akashauri ajiunge na NCCR–Mageuzi na CHADEMA na CUF tumuunge mkono. Ni yeye aliyemtambulisha Lowassa kwa waandishi wa Habari. Lipumba anajaribu kuiweka CUF sokoni, ili iinunue na itumiwe kuudhoofisha upinzani.

Lipumba amezoea na ameshaonja radha ya kutumika, alitumika mwaka 2010 akamsaidia Kikwete kushinda urais, mwaka 2015 alipoona hawezi kugombea urais akajua wanunuzi wataona hana thamani, akaona njia ni kujitoa kwenye chama ili wanachama wavurugike, mpango wake ukafeli vibaya kwani CUF ni taasisi. Wanunuzi wake, CCM, waanze kutafuta bidhaa nyingine kwa sababu CUF ilishamalizana naye. Waendelee kumpa ulinzi wa defender’ za Polisi, wampigie Saluti, wampe uenyekiti wa chama kwa nguvu ya dola n.k. Yote hayo hayataihamisha CUF kwenye ajenda zake katika kuwapigania Watanzania na Wazanzibari kwa ujumla.
Na mwisho sote tunaweza kuendelea kujiuliza swali la msingi, ni mahali gani Duniani kiongozi wa juu wa taasisi kubwa kama CUF ambaye aliwahi kuandika barua ya kujiuzulu na kuiacha ofisi yake kwa muda wa miezi kumi, taasisi ikachagua au kuteua kiongozi mbadala wa nafasi hiyo kisha baadae mtu huyo akalazimisha kurejea katika nafasi yake?

Mwisho:

Tunamtaka Lipumba ajiheshimu na kuacha kujidhalilisha kwa kulazimisha mambo ambayo hayawezekani na yaliyo kinyume na matakwa ya Katiba ya CUF. Chama chako kikishakukataa ndani ya chama, hata kama ungekuwa,na majeshi kutoka mwezini, huwezi kuwa kiongozi wa chama hicho. Tunamtahadhalisha Lipumba na wahuni wake kuwa watabeba Msalaba wa gharama zote zitakazotokana na uharibifu wowote wa mali za Chama utakaojitokeza. Yeye si wa kwanza kujaribu kutumika kutaka kuvuruga CUF na au vyama vya upinzani nchini lakini wote waliotumika muda wa kutumika ulipokwisha walitelekezwa na kufedheheka. Lipumba ashughulikie masuala yanayohusiana na fani yake ya uchumi kama alivyoaihidi wakati anajiuzuru, siasa imemshinda.

CUF imevuka vigingi vingi vizito katika nyakati tofauti kila ilipojaribiwa ikiwa kwa uadui wa ndani au wa nje, mwisho wa vitimbi vyote hivyo, CUF iliibuka mshindi. Tunatoa wito kwa wanachama, wapenzi wa CUF, na watanzania wote kwa ujumla waendelee kuwa na Subira. Hakika CUF ni taasisi makini na imara ya kisiasa nchini, na mwisho wa hili CUF ndiyo itakayoshinda.

"HAKI SAWA KWA WOTE"

YOWERI K. MUSEVEN HAS MOCKED HUMANITY

Yoweri Museveni has mocked humanity the manner in which history has never written before. We beseech the rest of the world to beware of nations run from the bedroom of a dictator.
 

Mwishoni mwa wiki iliyopita, watu zaidi ya 80 walipoteza maisha baada ya makabiliano kati ya walinzi wa Mfalme wa eneo la Rwenzururu Charles Mumbere na maafisa wa usalama.Je, hili ni tatizo la kisiasa ua kiusalama ? Victor Abuso anachambua suala hili kwa kina na Kenneth Lukwago akiwa jijini Uingereza na Brian Wanyama Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kibabii mjini Bungoma nchini Kenya.

 




picha za tukio la mauaji nchini Uganda