Wednesday, December 7, 2016


MATAPELI WAKUBWA WANNE (4)KUWAHI KUTOKEA TANZANIA : 

 
1..DAUDI BALALI... Nahisi huyu ni mmoja kati ya watanzania magenious zaidi kuwahi kutokea. Huyu kipindi anasoma alirushwa sana madarasa kutokana n kiwango kikubwa cha akili. Hii ilipelekea yeye kusoma elimu ya msingi na secondary kwa miaka 10 tu. Akiwa na miaka 18 alijiunga na chuo kikuu cha Howard marekani ambapo alitunukiwa shahada yake ya kwanza. Akiwa na miaka 25 alitunukiwa PHD.. Kisha akarudi nchini kuwa mchumi wa bank kuu mwaka 1967.. Baadae kidogo akaajiliwa IMF ambako alifanya kazi kwa miaka 23 kabla ya mkapa kumrudisha nchini kama mshauri wake wa masuala ya uchumi na baadae kumfanya gavana wa bank kuu.
Kilichofanya kuwepo kwenye list hii ni tukio alilofanya la ukwapuaji wa BILLION 164 za kitanzania pale bank kuu..
Nafahamu kuna theories nyingi sana kuhusu ufisadi wa EPA lakini kwa mujibu wa serikali ni kuwa BALALI alikula njama yeye na wale wafanyabiashara wakakwapua fedha pasipo serikali kujua, kwa maana hiyo BALALI alimpiga changa la macho Waziri mighiro, Rais, na hata usalama wa taifa..... ALIWEZA
2..MANYAUNYAU
Huyu jamaa tunafahamu alitikisa sana miaka ya 2006 hadi 2008 alijigamba kuwa akinywa damu ya Paka anapta uwezo wa kimiujiza kufichua wachawi. Alizunguka mitaa karibia yote ya uswahilini dar (uzunguni alipatenga) baada ya kuteka Hisia za watu vya kutosha akaanza na ziara za mikoani.
Jamaa akaingiza mkwanja mrefu sana kwa kazi yake hii nakumbuka miaka ile ya 2008 alishanunua RAV4 Kali na mjengo wa maana.... Sijui kwa sasa amepotelea wapi!
3..ALEX MASSAWE
Huyu jamaa ni tapeli(first class) alikuwa anatapeli kuanzia raia wenzake, serikali, mashirika mpaka matajiri wakubwa. Alitapeli sana watu nyumba, magari, mashamba na hata fedha, serikali iliangaika sana na huyu jamaa kwa miaka kadhaa lakini hawakufua dafu, mpaka interpol walipomkamata huko dubai.
Inasemekana jamaa alikuwa a napiga dili zake na watu wazito serikaln na bungeni. Inasemekana kuna wabunge watatu kutoka mkoa mmoja wa kaskazini ndio alikuwa anapiga nao sana ishu za madili ya gari za wizi na kusafisha fedha haramu..
4..BABU WA LOLIONDO
Mpaka Leo hii bado sijaelewa babu aliwezaje kuwapiga changa kiasi Kile, hivi ni kwamba babu alikuwa kichwa sana au media ilisaidia. Kipindi kile kuna watu walitamani BABU atangazwe kama nabii au shujaa wa taifa, mpaka wa kuu wa nchi walitengeneza hadi kiwanja kidogo cha ndege wakawa wanatua, wanapanga foleni, wanapiga magoti kwa unyenyekevu na kuachama midomo kama wanakula sakramenti takatifu.. Kila Kona ilikuwa BABU, BABU, BABUUUUU...
kila mtu kuanzia raia hadi viongozi wakubwa walikuwa wanapigania KIKOMBE kwa mchango (sadaka) ya mia tano tano (500)na ghafla ikawa ziiiiii Babu kimyaaaa




matukio ktk picha
 

No comments:

Post a Comment