Waziri wa afya wa Tanzania Bw Ummy Mwalimu ametahadharisha kuhusu mlipuko mpya wa ugonjwa wa kipindupindu nchini humo.
Bibi Mwalimu amewataka maofisa wa afya kutekeleza taratibu zinazolenga kusimamia maambukizi ya ugonjwa huo na kuanzisha kampeni ya kuelimisha umma kuhusu ugonjwa huo.
Ripoti mpya iliyotolewa na wizara hiyo inaonesha kuwa watu 6 wamefariki dunia na wengine 458 wameripotiwa kuambukizwa ugonjwa huo mwezi Novemba, na maeneo yaliyoathiriwa zaidi na Morogoro, Dodoma, Mara, Kigoma, Arusha na Dar es Salaam.
Bibi Mwalimu amesema ugonjwa huo hutokana na uchafu, na baadhi ya watu wana desturi ya kuchafua vyanzo vya maji.
![]() |
waziri ummi akizungumza na waandishi wa habari |
No comments:
Post a Comment