Monday, December 12, 2016

CHAMBUA MATAMKO YAFUATAYO...

#PART ONE:
1. WAZIRI WA VIWANDA, MWIJAGE "...tulikuwa tunaficha tu, ukweli ni kuwa DANGOTE anataka apewe GESI bure, nchi hii siyo shamba la Bibi"
2. WAZIRI WA NISHATI, MUHONGO "...DANGOTE hawasemi ukweli, gharama na Makaa ya Mawe ya Tanzania ni nafuu kuliko ya Afrika Kusini, hebu naomba wawaeleze ukweli"

3. TPDC: "...Shirika la Maendeleo la Petroli Tanzania (TPDC) linapenda kukanusha taarifa zinazoenezwa na Kampuni ya Dangote pamoja na washirika wake kupitia mitandao ya kijamii.....Kiwanda cha Dangote kimeomba kupewa gesi asilia kwa bei ambayo hapa kwetu Tanzania ni kidogo kwani kiasi hicho cha bei ndicho kinacholipwa kununulia gesi ghafi kutoka kisimani.... Taarifa hizo (Za Dangote) hazina mantiki yoyote na zinapaswa kupuuzwa...."

4. RAIS JPM: "...Kuna ujanja ujanja unatumika kumuuzia GESI Dangote kwa faida ya wachache, kuanzia sasa wasiliana na serikali moja kwa moja...."

5. DANGOTE: "...Hapakuwa na tatizo lolote, kila kitu kinakwenda sawasawa...".
#PART TWO:
1. WAZIRI MWIGULU NCHEMBA: "...miili iliyookotwa ni ya wahamiaji haramu..."

2. WAZIRI MKUU, KASIMU MAJALIWA: "Miili iliyookotwa inahusishwa na masuala ya Ugaidi..."
3. WAZIRI MKUU, KASIMU MAJALIWA: "Naagiza Uchunguzi mara moja (akiielekeza Wizara ya Mwigulu".

No comments:

Post a Comment