Monday, November 7, 2016

CHADEMA YAIGARAGAZA TENA POLISI ARUSHA.!



kwa hisani ya UKUTA Arusha

Jeshi la Polisi mkoani Arusha limepewa nusu saa (dakika 30) kuhakikisha limemfikisha Mbunge wa Arusha mjini Mhe.Godbless Lema Mahakamani. Amri hiyo imetolewa na Mahakama kuu mkoani humo kufuatia shauri lililofunguliwa na Mwanasheria wa Chadema, Wakili (msomi) Jonh Mallya aliyeiomba Mahakama hiyo kutoa amri ya kachiwa Lema kutoka mikononi mwa polisi ambapo anashikiliwa kwa muda wa siku 5 bila kupelekwa Mahakamani. Katika shauri hilo Mallya alisema Polisi wanamshikilia Lema kinyume cha sheria kwa muda wa siku 5 kwa madai kuwa mahojiano hayajakamilika. Mahakama kuu imekubaliana na hoja za Mallya na kuamuru Polisi kumfikisha Lema mahakamani hapo ndani ya nusu saa kuanzia sasa.

 

 

No comments:

Post a Comment