THE DEADLIEST SNAKE ON THE PLANET!
Anaitwa Mamba mweusi wa AfricaThe African Black Mamba!
Anapatikana katika Bara la Africa tuu...
Ndie nyoka hatari kabisa! Anatoa sumu aina mbili na zote ni noooma! Anatoa sumu inayojulikana kama "Neurotoxin hii huathiri mfumo wa neva
Napia anatoa sumu nyingine aina ya Cardiotoxin hii hushambulia mfumo wa moyo.... Nyoka huyu akikuuma unaweza kufa ndani ya dakika 20!
Black Mamba ninyoka mkorofi katili anasumu kali, anasifa ya urefu kama uavyomuona anafika hadi miguu 14 kwa hesabu za kiswahili! Ye huwa hana mwili mkubwa kama kina Python(Chatu) Mungu ni fundi sana huwa hakosei! Huyu nyoka ana roho mbaya sana kwanza amejaaliwa mbio kuliko nyoka wote! Ukikutana nae kuna ishara kuu mbili atakuonyesha kuwa Mimi African Black Mamba...Nyoka niliye jaaliwa sumu kuliko nyoka wote!
Ulaya hayupo huyu lakini Wazungu wanamtambua vema wakotaka kuja Afrika kuna viumbe kwanza wanaambiwa mkifika huko mnapaswa kuchukua tahadhari ya hali ya juu na viumbe hivi hatari.. Ktk list huyu nae yumo! So ukipata bahati yakukutana nae kwanza atakutisha! Ata achama kinywa ama mdomo wake wenye rangi nyeusi kwa ndani! Kinywa chake ni cheusi kwa ndani na ndio kimefanya aitwe Black Mamba!
Pili utamskia anatoa sauiti kama msela anaita demu! Au kama tairi linalotoa upepo...Tatu utamuona anatanua shingo yake japo sio kama ya Cobra!!! Hapo ujue uko mbele ya nyoka hatari kabisa! Uzidishe maombi! Vitu viwili usijethubutu kuvifanya! Moja... Uskimbie.. Maana huyu nyoka anambio zaidi ya Husein Bolt!
Mamba anakimbia Maili 12 kwa saa... Na akikukimbiza hakubali hadi akugonge sehemu ya mwili wako.. Ye ardhini huwa anateleza! Na ukimkimbia ni lazima tuu atakuunganishia! Na hatakukosa! Pili kuna wale watu akiona tu nyoka ye anakimbilia fimbo au jiwe... Siku ukutana na nyoka huyu jua umekwisha! Wataalam wanakwambia nyoka huyu hapigwi! Kwani hata hilo jiwe huenda usiwahi kulirusha au mfe wote!
Black Mamba anasifika kwa Show za kikatili anashambulia vibaya sana! Ndio maana nilisema Mungu ni fundi!
Pamoja na kumuumba nyoka huyu na Sumu kali mbio nyingi, hasira na urefu lakini nyoka huyu amejaaliwa huruma ndani yake ukikutana nae akianza kukuonyesha sarakasi zake kuwa mimi ndie nyoka hatari nawe Binaadam ukijishusha usikimbie wala ustupe jiwe ubaki unamuangalia tuu macho kwa macho! Unaambiwa atatuliza mzuka! Na wala hatakugusa ataingia zake mitini!
"Unaona Muumba alivyo wa ajabu"!!
Mamba anataga mayai kama kuku tuu kiota chake huwa ardhini...Jike anataga mayai 10-25 akishataga mayai yake huwa yanajiengua yenyewe baada ya miezi mitatu.
Joto ni muhimu kwaajili ya lncubation...na vitoto vyake vikisha jitotoa unaambiwa vinaanza mishe saa hiyohiyo hujitegemea kwa kilakitu! watoto wake wana sumu kali kama Mama yao yaani haina kuremba!!!
Nyoka huyu anaishi hadi miaka 11 porini... Akiwa anafugwa anaeza ishi hadi miaka 12......
No comments:
Post a Comment